DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA - News Today in World

DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA

DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA - Hallo World !!! News Today in World, In this article you read by title DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA, We've prepared this article well so you can read and retrieve information on it. Hopefully the contents of the post Article DAILY NEWS-HABARILEO, What we write can you understand. Okay, happy reading.


Title : DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA
link : DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA

newstoday-ok.blogspot.com ~

WATANZANIA kwa mara nyingine wamepata uhakika wa kushuhudia michuano mbalimbali mikubwa ya kimataifa baada ya DStv Kupitia SuperSport kuingia makubaliano ya kurusha michuano mikubwa ya kimataifa, ikiwemo michuano ya UEFA Euro 2020 pamoja na ile ya kufuzu UEFA Euro 2020  na pia michuano ya ulaya ya kufuzu kombe la dunia 2022 nchini Qatar.

Pia kuna lulu nyingine kwa watazamaji wa DStv hasa washabiki wa kandanda kwani pia mashindano mapya ya Ligi ya UEFA itakayoshindaniwa na timu kutoka nchi zote 55 ambazo ni wanachama wa UEFA. Michuano hii pia itakuwa ikionyeshwa katika  chaneli ya SuperSport.

Makubaliano haya yanawahakikishia watazamaji wa DStv kushuhudia michuano yote mikubwa ya soka  kila msimu hadi mwaka 2022.

“UEFA inafurahi kuendelea na kuimarisha uhusiano wake wa muda mrefu na supersport” amekaririwa Guy-Laurent Epstein, Mkurugenzi Mtendaji wa  UEFA Events SA. “Supersport  ni mshirika wa miaka nenda rudi wa UEFA na tunaimani kubwa kuwa SuperSport itaendelea kuwahakikishia watazamaji matangazo ya kiwango cha juu na pia amsha amsha  ya UEFA 2018-2022 kwa mamilioni ya watazamaji wa mitandange hiyo barani Afrika – Kusini mwa jangwa la Sahara.

UEFA Euro 2020, ni moja ya michuano itakayokuwa na shamrashamra nyingi ikizingatiwa kuwa itakuwa inatimiza miaka 60 tangu kuanza kwa michuano hiyo. Michuano hiyo itafanyika katika mini 13 ya nchi 13 tofauti barani Ulaya.

Michuano ya kufuzu ya Ulaya (The European qualifiers) itakuwa ya aina yake wakati ambapo nchi 55 zitakabana koo kuwania nafasi 24 za kushiriki michuano hiyo. Michuano hii ya kufuzu itaanza March 2019 hadi March 2020. 

“Hii ni mikataba mikubwa na muhimu sana” amesema Gideon Khobane, Afisa Mkuu wa SuperSport. “Michuano ya ulaya kwa kawaida huwa na mvuto mkubwa sana kwa  watazamaji wetu hivyo kuyafanya moja ya mashindano muhimu sanan. 

Tunaamini kuwa michuano hii inaendelea kuwa mikubwa na maarufu Zaidi hivyo bila shaka ushirikiano wa Supersport na UEFA utaongeza chachu katika michuano hiyo.


That's an article DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA

Fine for article DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA This time, hopefully can benefit for you all. Well, see you in other article postings.

You are now reading the article DSTV KUWAPA TENA RAHA WATANZANIA With link address https://newstoday-ok.blogspot.com/2017/06/dstv-kuwapa-tena-raha-watanzania.html

Subscribe to receive free email updates: